October 8, 2014


Beki wa zamani wa Simba, Victor Costa ‘Nyumba’, amejikuta akiingia katika hasara kubwa baada ya nyumba yake iliyopo Tegeta jijini Dar, kuteketea yote kwa moto usiku wa kuamkia jana Jumanne.

Masaibu hayo yamemkuta Costa wakati yeye akiwa mkoani Shinyanga na timu yake ya sasa ya Mwadui FC.
Costa amesema chanzo cha moto huo ni kibatari kilichowashwa baada ya umeme kukatika na baadaye moto wa kibatari kushika kwenye pazia na kwa kuwa watu hawakuwepo ndani, moto ule ulisambaa.
Costa aliongeza kuwa moto huo umeteketeza kila kitu kilichokuwa ndani ya nyumba na hakuna kilichosalimika.
“Moto umesababishwa na moto wa kibatari ulioshika pazia na baadaye kusambaa nyumba nzima, kulikuwa hamna mtu hivyo haukuzimwa kirahisi.
“Hakuna kitu kilichookolewa, moto umeteketeza kila kitu kilichokuwa ndani ya nyumba yangu,” alisema Costa.  

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic