October 8, 2014


Wachezaji wa Yanga wameanza kujiandaa jinsi ya kushangilia mabao watakapocheza mechi ya Watani wa Jadi dhidi ya Simba katika Uwanja wa Taifa, Oktoba 18.

Yanga na Simba watakutana katika mchezo wa Ligi Kuu Bara, huku Yanga ikiingia na historia ya kushinda michezo miwili kati ya mitatu ya ligi hiyo na Simba 
ikiwa bado haijapata ushindi wowote lakini haijafungwa.

Katika mazoezi ya Yanga, viungo washambuliaji, Haruna Niyonzima na Simon Msuva, ndiyo waliokuwa vinara wa kufanya zoezi hilo maalum la jinsi ya kushangilia mabao ambayo wataitandika Simba katika mtanange huo ambao umesalia siku kumi upigwe.

Viungo hao walitengeneza staili ya kukimbia katika kona ya uwanja na kujichezesha mabega huku mkono mwingine ukiwa kwenye mapaja. Wachezaji wenzao, Hassan Dilunga, Kelvin Yondani na Mrisho Ngassa walionyesha kuipenda hiyo staili huku wakifurahi jinsi Msuva na Niyonzima walivyoicheza.


Mechi ya Simba na Yanga ndiyo kubwa zaidi kuliko zote hapa nchini na imekuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa sana na mashabiki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic