Beki kisiki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’
amemshukuru Kocha Hemed Morogo kumteua kwenye kikosi cha Zanzibar Heroes.
Cannavaro ambaye amekuwa akiendelea kupaa kwa
kiwango kizuri, amesema Morocco amempa moyo kwa kuonyesha kudhamini mchango
wake.
“Najisikia faraja, pia namshukuru Morocco kwa
kuuona mchango wake kuwa unahitaji kwenye timu yangu.
“Najisikia faraja, nasikia nina deni la
kuwalipa Wazanzibar,” alisema Cannavaro ambaye sasa yuko na Yanga mkoani
Shinyanga wakijiandaa leo kuivaa Stand United.
Beki huyo na wenzake Aggrey Morris na Mwadini
Ally waliondolewa kwenye kikosi hicho na aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo,
Salum Bausi baada ya kugawana fedha za zawadi za ushindi wa tatu kwenye
michuano hiyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment