October 27, 2020


Anaandika Saleh Jembe


Bahati MBAYA, mchezo wa soka huwa hautoi furaha ya milele kwa UPANDE mmoja.


Tunaweza kujifunza msimu huu wa 2020/21 ikatusaidia kuongeza ufahamu kuhusiana na soka hata kama unaipenda vipi timu yako.


Ilikuwa vigumu kuamini Yanga ingeweza kuhimili mikikimiki hadi mechi angalau ya saba ikiwa imeshinda sita na sare moja kwa kuwa ilibadili nusu ya kikosi na ikaanza kwa kusuasua.


Azam FC walianza vema zaidi, wamepoteza kabla ya Yanga na Yanga wakishinda watakuwa juu yao. Simba yenye kikosi bora kwa kuchukua mara tatu mfululizo ubingwa, ndani ya mechi 7, wamedondosha pointi 8 huku wakipoteza pointi 6 katika mechi 2.


Hii inatoa funzo soka halitakupa kila unachotaka na hupaswi kuwa mwendawazimu au kuwehuka au kugombana na watu au kutukana hovyo kwa kuwa mchezo wa soka unapaswa ufurahiwe na wanaouelewa.


Angalia mwendo wa Yanga sasa, ni bora kabisa. Lakini hauwapi uhakika pia wa kila kitu, siku moja unaweza kubadilika na kuwa usiotarajiwa.


Soka mchezo wa kiungwana kwa maana ya kukubaliana na uhalisia na si uadui na chuki.


Tujifunze kukubaliana na nature ya mchezo wenyewe. Ukifungwa kubali, timu isipokuwa na performance nzuri tafakari, acha kukasirika na kulalama au kuwasingizia watu MANENO YA UONGO....


UKUMBUKE soka ni MGAWANYO WA FURAHA, leo UNASHINDA tu, kesho UTASHINDWA na yote yapokeee na kama unaona haiwezekani, basi CHAGUA MCHEZO MWINGINE WA KUUSHANGILIA.



7 COMMENTS:

  1. Ila hata nyie waandishi mulipitiliza kuwasifia simba au mulikuwa kazini kuisifia kwa maslahi yenu ilikuwa timu ya kawaida ila kila kituo simba simba

    ReplyDelete
  2. Waliwasifia Simba mpaka wakawatia Ujinga wachezaji,eti hata bila coach wanashinda, Sasa ndio matokeo yake.
    Kwakifupi msimu huu kiwago cha Simba kimeshuka

    ReplyDelete
    Replies
    1. Si walisema wao wenyewe kwamba "watawakera sana?"..ndo kero hizo zimeanza.
      Mgema wa kibongo imsifie hadharani? wallah atatia ruvu yoote

      Delete
  3. Haha hii ndio soka inafuraisha unakasirisha ina kushangaza

    ReplyDelete
  4. Kwa mara ya kwanza Saleh leo umeandika kitu cha maana sana kwetu sisi mashabiki wa hizi timu kubwa. Mchezo wa mpira ni katili kweli kweli. Yaani ni ngumu mno kukubali hiki kilicho ipata timu yangu pendwa Simba SC lakini ndio hivo tena; ni matokeo ya mpira hayo. Inabidi tujipange upya maana hakuna namna

    ReplyDelete
  5. Hahahaaaaa naona wameamua kwel kuwakera mashabik wao tuliwambia hao wazee itafika wakat watakuwa wamechoka na ndo dalili zmeanza na baaaaaado

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic