October 24, 2014


Kocha wa Makipa wa Klabu ya Simba, Zdravco Djekic, amesema foleni za Dar es Salaam zimekuwa zikimchosha na kumchanganya akili akihofia kuchelewa kushindwa kukamilisha programu zake za mazoezi.


Kocha huyo mgeni nchini, ni raia wa Serbia aliyekulia Afrika Kusini, amekuwa akiinoa Simba tangu Oktoba 10, mwaka huu wakati Simba ilipokwenda Afrika Kusini.

Kocha huyo alisema hajawahi kuishi kwenye jiji lenye foleni kama Dar, hivyo kukaa kwa muda mrefu kwenye foleni kunamfanya achoke na kumvuruga akili kitu ambacho siyo kizuri kwa kocha.

“Foleni za Dar zinanitisha sana, naogopa nisije siku nikafika wakati muda wa kumaliza mazoezi umefika. Tunakaa sana barabarani hadi mtu unachoka, ikiwa nitaishi karibu na uwanja wetu tunaofanyia mazoezi nitafurahi sana,” alisema Djekic.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic