| RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI |
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
limepuuza agizo la Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma
Nkamia la kusitisha suala la kuchukua fedha za klabu 14 za Ligi Kuu Bara na
kukutana na Bodi ya Ligi.
Badala yake, shirikisho hilo
limeendelea kupambana baada ya kumshitaki mwanasheria wa klabu hizo za Ligi Kuu
Bara, Dk Damas Ndumbaro kwenye kamati ya Nidhamu ya TFF.
Taarifa zinaeleza, Dk Ndumbaro
ametakiwa kufika kwenye kamati hiyo kesho ili kujibu tuhuma za yale
aliyozungumza kwenye vyombo vya habari.
Alichokizungumza Dk Ndumbaro ilikuwa
ni kupinga TFF kuzikata asilimia 5 klabu hizo kwenye fedha zao za udhamini.
Kama Waziri Nkamia ameagiza wakutane
Jumamosi halafu warudi serikali, halafu TFF imeamua kumshitaki mmoja wa
waliokuwa wakipinga ‘move’ yao ya kuzidhulumu klabu, maana yake imepuuza agizo
hilo.
Taarifaz a uhakika zinasema tayari Dk
Ndumbaro ameishapelekewa barua kutoka TFF ikimtaka kuhudhuria kikao cha kamati
ya nidhamu kitakachofanyika mchana wa kesho.
Blogu Hii inaendelea kufanya juhudi
kumpata Dk Ndumbaro kuhusiana na suala hilo ambalo lilionekana baada ya
serikali kuingilia kati kungekuwa na mwanga, lakini TFF imeonyesha jeuri yake.







Saleh una roho mbaya kama Tenga!
ReplyDelete