TFF
YAOMBA WADAU WABUNI JEZI MPYA YA TIMU ZA TAIFA
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linakaribisha wabunifu, kubuni mwonekano wa
jezi mpya za timu ya Taifa kwa mechi za nyumbani na ugenini. Ubunifu ni lazima
uzingatie rangi za bendera ya Taifa.
Mshindi
wa jezi ya nyumbani atapata sh. 1,000,000 (milioni moja), na mshindi wa jezi ya
ugenini atapata pia sh. 1,000,000 (milioni moja).
MBWANA SAMATTA AKIWA NDANI YA UZI WA SASA WA TAIFA STARS AMBAO PIA HUTUMIWA NA TIMU YA TAIFA YA SOMALIA. |
Ubunifu
utumwe kwenye anwani ya barua pepe: info@tff.or.tz au uwasilishwe kwa CD au
flash zikiwa katika mfumo wa PDF katika ofisi za TFF zilizopo ghorofa ya tatu
katika Jengo la PPF Tower, Mtaa wa Ohio na Garden Avenue. Mwisho wa kupokea
designs ni Novemba 15, 2014.
Kwa
maelezo zaidi unaweza kuwasiliana nasi kwa simu namba; 0713 210242 au 0714 634838.
0 COMMENTS:
Post a Comment