December 7, 2014

 
EMERSON.
Kiungo wa Yanga, Emerson Roque na mshambulia mpya wa Simba, Danny Sserunkuma raia wa Uganda wakatakutana siku ya mechi ya Bonanza la Mtani Jembe kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Yanga ilimzuia Emerson raia wa Brazil kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Express, jana. Lakini Simba nayo imemuweka jukwaani Sserunkuma leo wakati inapambana na Mtibwa Sugar katika mechi ya kirafiki ndani ya Dimba la Chamazi jijini Dar.

Maana yake wawili hao watakutana katika mechi hiyo ya kirafiki.
Kuna uwezekano mkubwa wa kupambana kwa kuwa Sserunkuma ni ‘mtamu’ zaidi anapocheza namba kumi.

Wakati Emerson ameonekana kuwa anatulia zaidi akicheza kiungo mkabaji, yaani namba sita.

Kutokana na namba zao, maana yake wawili hao watapambana vilivyo siku hiyo.


Mechi hiyo inasubiriwa kwa hamu kwa kuwa kila upande una wachezaji kadhaa wapya na tayari Makocha Marcio Maximo na Patrick Phiri wamekutana mara moja msimu huu na matokeo yakawa suluhu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic