December 3, 2014

RUVU
Klabu ya Ruvu Shooting ya Pwani, imeamua kumwaga nyota watano kwa mpigo katika harakati za kutafuta mastraika, safu ambayo imewasumbua kwa muda mrefu tangu kuondoka kwa Elias Maguli aliyetimkia Simba.


Ofisa Habari wa Ruvu, Masau Bwire, alisema nyota hao tayari wameanza majaribio tangu juzi Jumatatu ambapo wataangalia wenye uwezo zaidi kabla ya kuwapa saini.

Bwire amesema kuwa wameamua kuvalia njuga safu hiyo kwani ndiyo iliyoonyesha matatizo zaidi katika mechi saba za mzunguko wa kwanza.

“Kuna wachezaji watano wameanza mazoezi na kikosi chetu, wanatokea timu ndogo, wapo kwa ajili ya majaribio ambapo kocha Tom Olaba atapata nafasi ya kuchagua nani atavutiwa naye.

“Tumeamua kuleta mastraika maana ndiyo sehemu iliyotutesa zaidi na ikumbukwe kuwa kuna wachezaji wetu kama saba ambao wamekwenda kwenye mafunzo ya kijeshi, hivyo tunataka kuziba mapengo yao,” alisema Bwire ambaye pia ni Mwenyekiti wa Uchaguzi wa Chama cha Soka Mkoa wa Pwani (Corefa).



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic