December 3, 2014


Kiungo mshambuliaji mpya wa Simba, Omar Mboob, ambaye yupo kwa ajili ya majaribio katika kikosi hicho, amekabidhiwa jezi namba 28 atayokuwa anaitumia ambapo jezi hiyo ilikuwa inamilikiwa na kiungo, Amri Kiemba ambaye ametimkia Azam FC.


Mboob raia wa Gambia ameanza mazoezi na kikosi hicho cha Wekundu wa Msimbazi juzi Jumatatu katika Gym ya Chang’ombe, Dar es Salaam.


Msemaji wa timu hiyo, Humprey Nyasio, alithibitisha kiungo huyo kukabidhiwa jezi hiyo ambapo alisema atakuwa kwenye majaribio katika kikosi hicho kwa muda wa wiki mbili.

“Ni kweli Mboob amekabidhiwa jezi ya zamani ya Kiemba (namba 28) ambapo tunatarajia kuwa naye katika kikosi chetu kwa takribani wiki ambapo atakuwa anafanya majaribio,” alisema Nyasio.

Kama Mboob akifanikiwa kufuzu majaribio katika timu hiyo, itawalazimu kumtema mchezaji mmoja wa kimataifa kutokana na kupita idadi ya wachezaji watano iliyowekwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic