January 21, 2015


Straika wa zamani wa Yanga, Mkenya, Boniface Ambani, amekikubali kiwango cha kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Mbrazili, Andrey Coutinho, huku akimshauri kuingia gym.


Kauli hiyo, aliitoa mshambuliaji huyo mara baada ya kumalizika kwa mechi ya Ligi Kuu Bara iliyowakutanisha Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kumalizika kwa suluhu.

Ambani ambaye sasa ni mfanyabiashara alisema kuwa kiungo huyo amepungukiwa vitu vichache pekee ambavyo vinarekebishika kama akihitaji, ambavyo ni nguvu na pumzi ya kutosha.

Ambani alisema, kiungo huyo anatakiwa kufanya mazoezi yatakayomuongezea vitu hivyo, ikiwemo kuingia gym na kukimbia ufukweni kwa ajili ya kujiweka fiti.
“Nikwambie ukweli tu, Yanga wamesajili vizuri sana na hiyo ni kutokana na ubora wa kila mchezaji kwa jinsi nilivyowaona kwenye mechi yao dhidi ya Ruvu Shooting ambayo ilimalizika kwa suluhu.


“Ukiangalia mchezaji kama yule Mbrazili (Coutinho) ni mzuri ana kiwango kikubwa, lakini ana upungufu mdogo ambao unarekebishika wa kukosa stamina na nguvu pekee, nikuhakikishie kama akifanikiwa kuvifanyia kazi vitu hivyo, basi atakuwa tishio, niamini mimi,” alisema Ambani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic