January 21, 2015


Baada ya kuandamwa na vipigo mfululizo katika ligi kuu, uongozi wa Ndanda FC umeibuka na kuomba msamaha kwa mashabiki wake.


Timu hiyo wikiendi iliyopita iliambulia kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Simba, katika uwanja wao wa nyumbani wa Nangwanda Sijaona na mpaka sasa ipo nafasi ya pili kutoka mkiani ikiwa na pointi kumi pekee.

Msemaji wa timu hiyo, Idrisa Bandari, alisema kuwa si kwamba wao wanapenda kupoteza kila mchezo, bali ni aina ya matokeo ambayo yanawatokea kama sehemu ya mchezo.

 “Mashabiki wetu watusamehe kwa matokeo mabaya, si kwamba tunapenda kuwa hivyo, timu inajituma sana, tunapata nafasi lakini hatuna bahati kabisa pia ligi imekuwa ngumu sana kwa sasa.

“Lakini wasikate tamaa, waendelee kutusapoti kuhakikisha tunapiga na kuweza kufanya vyema ingawa ushindani unazidi kuwa mgumu,” alisema Bandari.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic