Mshambuliaji Mario
Balotelli haishi vituko, sasa amemtema mpenzi wake mwanamitindo Fanny Neguesha.
Kisa cha Balotelli kumtema
mwanadada huyo mwanamitindo, eti hapendi apige zile picha dizaini kama
zinaonyesha mwili wake sana.
Lakini pia kuna picha ya ‘mijibaba’
ikiwa imemkumbatia, yeye hataki kuamini hiyo ni kazi.
Balotelli alikuwa
ameishamvisha pete yenye thamani ya pauni 25,000 lakini inaelezwa Fanny ambaye
asili yake ni Nigeria ameisharudisha pete hiyo.
Ukiangalia ukurasa wake wa
Instagram, mwanadada huyo anatembea mji mmoja baada ya mwingine na picha ndiyo
mambo yake.
Mzee mzima Ballo amesema
haiwezekani, dada aliposhikilia msimamo wake, kampiga chini.
0 COMMENTS:
Post a Comment