Na
Saleh Ally
MWAKA
1972 mchezaji nyota wa Zaire (sasa DR Congo), Tshmeni Bwanga alishika nafasi ya
pili ya Mchezaji Bora wa Afrika, mshindi alikuwa Cherif Souleyman wa Guinea.
Mwaka
uliofuatia Bwanga akaibuka kuwa Mchezaji Bora Afrika, akifuatiwa na Mwamba
Kazadi wa Zaire pia na wote hawa wawili walikuwa wanakipiga katika kikosi cha
TP Mazembe.
Mwaka
1974 ambao ulikuwa ni wa tatu, tuzo hiyo ikaenda kwa Paul Moukila wa Congo
Brazzaville, nafasi ya pili Lobilo Boba wa Zaire na tatu Hassan Shehata wa
Misri ambaye baadaye amekuja kuwa kocha maarufu wa nchi hiyo.
Historia
hiyo kwa ufupi, haina utamu wowote kwa Mtanzania kwa kuwa hakuna kinachomgusa
zaidi. Ila inaweza kuzua maswali kwamba kumbe DR Congo wamekuwa hadi kwenye
nafasi za mchezaji bora Afrika na wamewahi kuitwaa tuzo hiyo.
Hiyo
ni sehemu ya ukanda wetu, hata jirani zetu Zambia kupitia Kalusha Bwalya mwaka
1988, halafu 1989, akawa wa tatu mshindi akiwa Joseph-Antoine Bell wa Cameroon.
Tuzo
za mchezaji bora mwaka huu, katika majina ya mwisho wale 25 kabla ya fainali
yenyewe, Tanzania haina mchezaji hata mmoja.
Lakini
kuna listi ya wachezaji 20 ambao watawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa
wale wanaocheza ndani ya bara hili, Tanzania haina hata mchezaji mmoja!
Uganda:
Unaweza
kusema huko ni kugumu sana, lakini katika wachezaji hao 20 walioteuliwa kuwania
tuzo hiyo kwa wachezaji wanaocheza barani Afrika, jirani zetu Uganda wana
wachezaji Yunus Sentam anayekipiga AS Vita ya DR Congo na Geoffrey Massa
anayeichezea Pretoria University ya Afrika Kusini.
Katika
listi hiyo, DR Congo ina wachezaji wanne, sasa jiulize kwa nini Tanzania tangu
enzi hizo haina mchezaji hata mmoja anayewania tuzo hizo?
Kipimo
au ubora wa soka ya Tanzania upo wapi? Tutasema, tutaelezwa na kudanganywa hadi
lini?
Maswali
rahisi, majibu yake ni vigumu kupatikana kwa kuwa wahusika wala hawana habari.
Diamond:
Majibu
itakuwa shida, lakini tukumbushane sasa kwamba Tanzania nayo itakuwa sehemu za
tuzo hizo zitakazofanyika Januari 8 jijini Lagos, Nigeria.
Kijana
huyo anastahili sifa, hakuna ubishi kwamba hajafika hapo kwa nguvu za giza,
amejituma, amebuni, amepambana nyumbani, Afrika, Ulaya hadi Amerika. Sasa
anakubali.
Hatujui
yupi kutoka nchi ipi atashinda katika tuzo hizo za Shirikisho la Soka Afrika
(Caf), lakini ubora wa msanii wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’ ndiyo
utakaotuwakilisha.
Hakuna
ubishi tena, tuzo hizo ni za ubora. Wanaowania lazima wawe bora. Wageni wengi
waalikwa ni waliowahi kuwa bora, shujaa wa nchi zao.
Hata
watakaotumbuiza, ni wale wanaoonekana kuwa na kiwango bora kinachokubalika
Afrika.
Diamond
amevuka kwenye suala la rekodi hadi kwenye soka. Huenda Caf wangetamani
kumwalika au kumshirikisha hata mmoja katika soka, nani sasa?
Diamond
ndiyo mwakilishi na hakuna ubishi anakwenda kwenye tuzo hizo kupitia ubora
wake. Tujivunie, ndiyo. Lakini kwa wadau wa soka, lazima tuone aibu, ndiyo!
DR
Congo imeanza kufika huko tangu enzi za Zaire, usisahau kwa muziki pia hatuwapati.
Zambia pia ambao ni jirani zetu, yaleyale. Leo Uganda nao, wanakwenda huko mara
kibao, mwisho utasikia Rwanda, Burundi, sisi tuko hapahapa ‘chai’ nyingi na
programu zisizokamilika.
Viongozi
wa Yanga, Simba na klabu nyingine acheni blah-blah. Jifunzeni, fanyeni mambo
yanayoangalia Bara la Afrika. Kufungana nyie imetosha, kuwa na viongozi
wanaotaka sifa pia imetosha. Sasa ni malengo na mafanikio kimataifa.
Timu
za Tanzania zikifika mbali kimataifa hasa barani Afrika, hakuna ubishi
wachezaji bora wataanza kupatikana.
Kwa
wachezaji pia, acheni uvivu, acheni uoga wa kupambana na changamoto. Nendeni
mkacheze nje kama wanavyofanya wenzenu wa Uganda, hivyo ndiyo njia rahisi ya
kuleta mafanikio nyumbani.
Leo
mnajisifia Diamond kufika hapo, lakini naye angekubali kama nyie akabaki
kitumbuiza Tandale, Sinza, Mbagala, Ilala na kwingineko, naye asingefika hapo
alipo.
Yanga,
Simba na wenzao tatizo, wachezaji wao na wameridhika, mashirikisho hasa baba
yao, TFF, nao tatizo kubwa!
Hebu
hata kidogo muwe mnaumizwa na mafanikio ya wengine. Halafu muweze hata
kujiuliza na kubadilisha mambo. Hivi nyie ni watu wa aina gani!!
BAADHI
YA WALIOTWAA TUZO ZA MCHEZAJI BORA AFRIKA:
MCHEZAJI NAFASI YA 1 2 3
Samuel
Eto'o (Cameroon)
4 2 2
George
Weah (Liberia)
3 4 0
Abedi
Pelé (Ghana)
3 0 0
Yaya
Touré (Ivory Coast) 3 0 0
Didier
Drogba (Ivory Coast) 2 4 3
Roger
Milla (Cameroon)
2
2 1
Thomas
N'kono (Cameroon) 2 1 1
Nwankwo
Kanu
(Nigeria) 2 0 0
El
Hadji Diouf (Senega)
2 0 0
Rashidi
Yekini (Nigeria)
1 1 1
Emmanuel
Amuneke (Nigeria) 1 1 0
Tshimen
Bwanga (DRC) 1 1 0
Kalusha
Bwalya (Zambia) 1 0 1








0 COMMENTS:
Post a Comment