Kamati
ya Mpira wa Miguu wa Wanawake ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
imetupa rufani ya timu ya Mwanza kupinga uhalali wa wachezaji wawili wa Kigoma
kwenye mechi yao ya robo fainali iliyochezwa jana (Januari 26 mwaka huu) Uwanja
wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Mwanza
iliyopoteza mechi hiyo kwa mabao 2-1 iliwalalamikia wachezaji Neema Sanga na
Vene Dickson wa Kigoma kuwa waliwahi kuchezea timu ya Taifa (Twiga Stars),
hivyo kucheza mashindano ya Kombe la Taifa la Wanawake ni kinyume cha kanuni.
Kamati
baada ya kupitia rufani hiyo, imeitupa kwa vile timu ya Mwanza haikuwasilisha
vielelezo vyovyote kuthibitisha madai hayo dhidi ya wachezaji hao. Pia Kamati
yenyewe ilipitia taarifa za Twiga Stars ambapo haikupata kumbukumbu za
wachezaji hao katika timu hiyo.
Pia
Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake ya TFF imesikitishwa na kitendo cha
viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) Mkoa wa Mwanza
kugomea uamuzi dhidi ya rufani yao, hivyo imependekeza Mwenyekiti wa TWFA
Mwanza, Sophia Tigalyoma na Katibu wake Hawa Bajanguo wapelekwe Kamati ya
Nidhamu kwa hatua za kinidhamu.
0 COMMENTS:
Post a Comment