Kocha
Mkuu wa Ruvu JKT, Fred Felix Minziro amesema wataonyesha burudani ya kutosha
katika mechi yao ya leo dhidi ya Simba.
Minziro
amesema anajua Simba watakuwa wamejiandaa baada ya kufungwa katika mechi
iliyopita dhidi ya Mbeya City.
“Tunajua
Simba watakuwa wamepania kufanya vizuri, lakini hata sisi tunataka kushinda
baada ya kumaliza kwa sare katika mechi iliyopita.
“Tumejiandaa
na utaona, kwa kuwa tumepanga kushambulia,” alisema Minziro.
Katika
mechi ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye Uwanja wa Taifa na Simba ikalala
kwa mabao 3-2.
Ruvu JKT
ina pointi 18 na inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Bara.
0 COMMENTS:
Post a Comment