January 10, 2015


Vinara wa Ligi Kuu Bara, Mtibwa Sugar wameimeng’oa JKU na kutinga fainali ya Kombe la Mapinduzi.


Mtibwa imetinga fainali baada ya kulazimika kuingia kwenye changamoto ya mikwaju ya penalti baada ya kumaliza muda wa kawaida kwa sare ya bila kufungana.

Ushindi wa penalti 4-3 ndiyo ulioipeleka Mtibwa Sugar ambayo beki wake David Luhende pekee ndiye alipoteza mkwaju wake kwa kupiga nje.

Wachezaji wawili wa JKU nao walipaisha mikwaju yao na kumpa nafasi Vicent Barnabas kuwamaliza.

Sasa Mtibwa inamsubiri mshindi kati ya Simba dhidi ya Polisi Zanzibar leo usiku.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic