Beki Juma Nyosso wa Mbeya City amesema amefurahishwa na ushindi walioupata dhidi ya Simba lakini pia uwezo aliouonyesha katika mechi hiyo wikiendi iliyopita.
“Unapocheza na timu yako ya zamani lazima uwaonyeshe kuwa bado upo bora kiasi gani,” hiyo
ni kauli ya beki wa Mbeya City, Juma Nyosso aliyoitoa baada ya timu yake
kuifunga Simba mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu Bara, juzi.
Simba
ilipata kipigo hicho kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, huku Nyosso ambaye ni beki wa
zamani wa Simba akiwa nahodha wa Mbeya City.
“Nimefurahi
tumeshinda kwenye mchezo mgumu kama huu na usiotabirika lakini kuhusu kucheza na
timu yangu ya zamani ni kitu kizuri zaidi kwa kuwa unapata nafasi ya
kuwaonyesha kuwa bado upo bora kwa kiwango gani na nashukuru nimefanikiwa
kulifanya hilo.
“Nimewaonyesha
viongozi wa Simba kuwa walifanya makosa makubwa ya kuniacha wakidai nimeshuka kiwango,”
alisema Nyosso.
0 COMMENTS:
Post a Comment