January 30, 2015


Uongozi wa Klabu ya Yanga umesema unatarajia kuwasilisha barua kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jumatatu ijayo kuomba mchezo wao dhidi ya Mtibwa Sugar wa Februari 8, usogezwe mbele.


Yanga inatarajiwa kukipiga na BDF XI ya Botswana katika Kombe la Shirikisho mnamo Februari 14 lakini inatakiwa itekeleze majukumu yake katika Ligi Kuu Bara, Februari 8.

Katibu wa Yanga, Jonas Kiboroha amesema hii: “Tumeandaa barua ambayo tutaipeleka TFF siku ya Jumatatu kuomba mchezo wetu dhidi ya Mtibwa usogezwe kwa lengo la kupata muda wa kujiandaa kabla ya kuivaa BDF XI.”

Wakati huohuo, Yanga ipo katika mazungumzo na timu ya Vipers ya Uganda kwa ajili ya kucheza nao mchezo wa kirafiki kabla ya kuvaana na BDF XI.

Mkuu wa Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro, ndiye aliyetoa tamko kwa kusema: “Tupo katika mazungumzo na Vipers lakini hatuwezi kusema lini tutacheza nao rasmi kwa kuwa bado mazungumzo yanaendelea.”




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic