Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)l imepokea kwa masikitiko taarifa za kuwepo
tena kortini kwa kesi dhidi ya uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar
(ZFA), jambo ambalo linaweza kuathiri ushiriki wa timu za Zanzibar kwenye Ligi
ya Mabingwa Afrika, na Kombe la Shirikisho.
Mwishoni
mwa mwaka jana, TFF ilihadharisha juu ya masuala ya mpira wa miguu kupelekwa
mahakamani, kwani kwa mujibu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu
(FIFA) kitendo hicho ni kinyume cha taratibu za uendeshaji mpira wa miguu
ambazo zinakataza masuala ya mchezo huo kupelekwa katika mahakama za kawaida.
Kutokana
na hali hiyo, TFF iliiandikia barua ZFA kutaka mgogoro huo uondolewe kortini na
yenyewe kuridhia kuwa tayari kupeleka ujumbe Zanzibar ili ukutane na pande
zinazohusika.
Pia
TFF ilisema timu za Tanzania Bara zisingeruhusiwa kushiriki michuano ya Kombe
la Mapinduzi 2015 iwapo kesi hiyo ingeendelea kuwepo kortini na kutaka
iondolewe bila masharti yoyote.
ZFA
iliithibitishia TFF kuwa kesi hiyo imeondolewa kortini bila masharti, hivyo
timu za Tanzania Bara kuruhusiwa kushiriki katika michuano ya Kombe la
Mapinduzi. Ni muhimu suala hilo likashughulikiwa haraka ili kutohatarisha
ushiriki wa timu za KMKM na Polisi kwenye michuano hiyo ya Shirikisho la Mpira
wa Miguu Afrika (CAF).
0 COMMENTS:
Post a Comment