January 5, 2015


Kocha wa makipa wa Yanga, Juma Pondamali amepigwa marufuku kujihusisha na shoo za muziki mpaka pale ligi kuu itakapomalizika msimu huu.


Kocha huyo asiyeishiwa vituko, amekuwa akijihusisha na masuala ya muziki na mpaka sasa ameshatoa ‘singo’ kadhaa ikiwemo Domo la Mamba na nyingine kibao.

Kocha huyo alisema amepigwa marufuku na uongozi wa timu hata kama kuna sikukuu, biashara za kwenda kufanya shoo na kupanda jukwaani zisifanyike kwa sasa.

Pondamali alifunguka zaidi na kudai hana jinsi inabidi asikilize viongozi wake wanataka kitu gani, hivyo mashabiki wake wamsubiri kwanza.

“Kwa sasa viongozi wangu hawataki kabisa kusikia wala kuniona jukwaani nafanya shoo hata kama kuna sikukuu au nimepata mualiko, zaidi wamesema nisubiri tu mwezi Mei ambapo ligi itakuwa imesimama.


“Kwa hiyo kwa sasa hakuna kinachoendelea, hivyo nasubiri hiyo Mei ligi itakapomalizika ndiyo nitarudi mzigoni kuendelea na majukumu yangu ya kutoa album na video za nyimbo zangu,” alisema Pondamali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic