Baada ya kufanikiwa kufumania nyavu kwa mara
ya kwanza, straika mahiri wa Polisi Moro, Said Bahanuzi, amefungua kinywa na
kusema kuwa amefurahi sana kuipa heshima klabu yake mbele ya Mbeya City.
Timu hizo zilikutana wikiendi iliyopita katika
mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Morogoro, ambapo Polisi Moro
iliilaza Mbeya City kwa bao 1-0.
Bahanuzi
amesema kuwa amefurahi kufunga bao hilo pekee katika mchezo ambao ulikuwa na
ushindani wa hali ya juu, hivyo atahakikisha anafanya jitihada za kuendelea
kuisapoti timu hiyo.
“Mchezo ulikuwa mgumu sana, kikubwa namshukuru
Mungu kwa kunipa uwezo wa kufunga bao moja tena la pekee mbele ya wapinzani
wetu Mbeya City, naamini hiyo ni heshima tosha kwa upande wangu.
“Msimu huu ligi ni ngumu sana tofauti na miaka
ya nyuma, lakini nitahakikisha natoa mchango wangu wa hali na mali ili
kuinusuru timu yetu katika panga la kushuka daraja,” alisema Bahanuzi.







0 COMMENTS:
Post a Comment