February 26, 2015


Msanii hip hop, Rashid Makwiro 'Chid Benz' amehukumiwa miaka miwili kwenda jela.



Hukumu hiyo imetolewa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu jijini Dar es Salaam ambako kesi yake ya kukamatwa na madawa ya kulevya ilikuwa inasikilizwa.

Hukumu ilikuwa ni adhabu ya miaka miwili jela au kulipa faini ya Sh 9,000,000 ambayo aliilipa baada ya watu wake kujitokeza na kukamilisha hilo na sasa Chid Benz.

Kesi yake hiyo iliyoendeshwa kwa wiki kadhaa, ilitokana na msanii huyo kukamatwa na madawa ya kulevya kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere akiwa njiani kwenda mjini Mbeya kwa ajili ya shoo.

Chid Benz alikiri madawa aliyokamatwa nayo kwenye mfuko wa shati yalikuwa yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic