Licha ya kwamba Kampuni ya Bin Slum Tyres
Ltd kuachana na Coastal Union, lakini mashabiki kibao wa timu hiyo walivaa jezi
zenye nembo ya kampuni hiyo.
Licha ya Coastal Union kupoteza kwa bao 1-0
dhidi Yanga kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, mashabiki hao walizidi
kuonyesha mapenzi yao kwa timu hiyo wakiwa na jezi za Bin Slum tena
wakishangilia kwa aina yao.
Walikuwa wakigeuka na kuanza kuonyesha
migongo yao huku wakiwa na baadhi ya mabango, moja likisomeka “Tanga kwanza”.







0 COMMENTS:
Post a Comment