Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limekuwa likichukua hatua kutokana na matukio ya vurugu
katika Ligi Daraja la Kwanza lakini inavyoonekana kazi bado ni ngumu kukomesha
vurugu kutokana na matukio mengi ya ajabu yanayoendelea kutokea kwenye michezo
ya ligi hiyo.
Vurugu
zilizotokea kwenye mechi ya Toto Africans dhidi ya Geita Gold Sports kwenye Uwanja
wa Shule ya Sekondari Nyankumbu na ile ya Mwadui dhidi ya Polisi Tabora,
zinatoa picha kuwa bado kuna vitu havipo sawa.
Geita
vs Toto
Awali,
mashabiki wa Geita walionyesha chuki ya wazi kwa wenzao wa Toto kwa kuwaambia
lazima wawapige.
Baada
ya mchezaji wa Geita, Venance Joseph kuunawa mpira katika dakika ya 14 na
mwamuzi kuamuru penalti, kilichotokea baada ya hapo ni vurugu kubwa, mashabiki
kuvamia uwanja, polisi kupambana na mashabiki na mwamuzi kupigwa kichwa na
mchezaji wa Geita.
Licha
ya uwepo wa viongozi wa serikali katika mchezo huo, mazingira ya uwanja huo pia
ni hatarishi kwa usalama wa wachezaji na wahusika kwa kuwa hauna sifa za
kuchezewa mechi kubwa na yenye ushindani ambayo inaweza kuhudhuriwa na
mashabiki wengi.
Kuna
hatua mchezaji wa Toto, alipigwa na jiwe kubwa mgongoni kiasi cha kupoteza
fahamu kwa dakika kadhaa.
Polisi
nao wakaanza kukimbizana na mashabiki kama vile vitani, hakika ilikuwa hali ya
kusikitisha na hofu kubwa.
Mwadui
FC vs Polisi Tabora
Dalili
za vurugu zilianza kuonekana kabla ya mchezo huo kutokana na kuonekana kwa
dalili za kushutumiana katika imani za kishirikina, mfano ni kitendo cha Polisi
Tabora kuzuiwa kuingia uwanjani kwa muda.
Wakati
mchezo ukiendelea, kulitokea vurugu za mashabiki wa timu hizo mbili, huku
mashabiki wenye umri mdogo nao wakiwemo uwanjani, wengine wakiwa wameshika
vilevi vilivyomo ndani ya chupa.
Mchezo
huu haukuwa na vurugu nyingi lakini bado mazingira ya kiusalama hayakuwa mazuri
kwa wahusika wote waliofika kushuhudia mechi hiyo.
Mtazamo
Inavyoonekana
bado kuna tatizo kubwa kwenye suala la uelewa wa mashabiki wa baadhi ya mikoa,
mazingira ya rushwa hasa kwa waamuzi ni makubwa, mazingira ya viongozi wa mikoa
kubeba timu zao yamekithiri, waamuzi kutokuwa salama pia ni suala kubwa.
TFF na wadau wote tunatakiwa kuwa
kitu kimoja katika kukemea na kuondoa madudu yanayoendelea kwenye soka letu,
kwani ukimya au kulea yote hayo, matokeo yake ni kuzalisha matatizo makubwa
zaidi.









0 COMMENTS:
Post a Comment