February 27, 2015


Uongozi wa klabu ya Stand United nao umeibuka na kudai kuwa unashindwa kujua ni wapi ukashitaki kutokana na hujuma walizofanyiwa na kusababisha mapato kuwa madogo.


Stand ambayo ilicheza na Simba, wikiendi iliyopita imelalama kuwa kuna watu ambao wamo kwenye mamlaka za soka nchini ndiyo ambao wamekuwa wakihusika katika hujuma mbalimbali.

Klabu hiyo inadai kuwa kuna watu ambao wamo ndani au wamekuwa wakifanya kazi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), wamekuwa wakizinyonya klabu na mfano halisi ni juu ya mapato ya mechi yao dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Katika mchezo huo, mapato yaliyotangazwa na TFF ni shilingi milioni 31, Stand ikaambulia milioni 6.5 huku Simba ikipata milioni 4.6.

Katibu Msaidizi wa Stand, Kennedy Nyagi, amesema walitafuta njia mbadala ya kudhibiti mapato katika mechi hiyo lakini wakapigwa vita na watu ambao alidai wanawategemea katika kuziendeleza klabu.

“Inaumiza sana, watu ambao tunawategemea ndiyo wanatuangusha, mapato tuliyopata mchezo wetu na Simba hayafanani. Wameuza mpaka vishina vyote, maana tiketi zimeuzwa mara tatu. Viongozi wanaodaiwa ni wa TFF na Bodi ya Ligi walikuwepo pale, tulitoa mawazo yetu ili kuweza kunusuru ubadhilifu lakini wao wakawa wanapinga.


“Inakuwa ngumu kwenda kulalamika hasa kwa vyombo husika wakati wao ndiyo wanakuwa chanzo cha matatizo,” alisema Nyagi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic