RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI. |
Kamati
ya Utendaji ya Shrikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyokutana Jumapili
Februari 22 mwaka huu, imefanya mabadiliko ya mahali utakaofanyika Mkutano Mkuu
wa mwaka kutoka Mkoa wa Sinigida na kuhamishia mkoa wa Morogoro.
Hatua
hiyo imefikiwa na Kamati ya Utendaji kutokana na sababu za kutokukamilika kwa
miundombinu ya mkutano mkuu na kuwepo ka shughuli nyingine za kijamii mkoani
humo.
Kamati
ya Utendaji inamshukuru Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Singida
(Sirefa), na uongozi mzima kwa kujitolea kuandaa mkutano huo na huko nyuma
waliweza kuandaa mkutano wa makatibu wa vyama vya soka vya mikoa.
TFF
itaandaa vikao na matukio mengine mkoani Singida itakapotokea hapo baadae,
tarehe ya mkutano mkuu itaendelea kubakia ile ile ya Machi 14, 15 mwaka huu.
0 COMMENTS:
Post a Comment