Klabu ya Simba isipokuwa makini katika kuwaongezea wachezaji wake 11 mikataba, basi huenda ikawapoteza nyota 11 ambao wengi wao ni tegemeo kwenye kikosi cha Mserbia, Goran Kopunovic.
Simba imeonekana kusuasua msimu huu lakini pia
ina hali ngumu kwa kuwa wachezaji wake 11 wanamaliza mikataba yao mwishoni mwa
msimu huu.
Simba inaweza kuwapotezea wachezaji wao kwenye
kikosi cha Yanga ambacho kimekuwa kikiwawinda baadhi ya wachezaji wa timu hiyo
kwa kipindi tofauti.
Wachezaji hao ambao mikataba yao inatarajiwa
kumalizika ni Ivo Mapunda, Said Nassor ‘Chollo’, Joseph Owino, Issa Rashid ‘Baba
Ubaya’, Said Ndemla na Haroun Chanongo.
Wengine ni Shaaban Kisiga, Adam Miraji,
Abdallah Seseme, Hassani Isihaka na William Lucian ‘Gallas’ ambao wote hivi
sasa wanaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine kwa mujibu wa kanuni za
Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kwa kuwa wamebakiza chini ya miezi sita.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani
ya uongozi wa timu hiyo, kamati ya usajili ya timu hiyo, tayari imeanza
mazungumzo ya awali na baadhi ya wachezaji wanaowahitaji kwa ajili ya msimu
ujao wa ligi kuu.
Chanzo hicho kilisema, uongozi utawabakiza
wachezaji hao wanaowataka baada ya kumtathmini kila mmoja kulingana na mchango
wake katika timu na mahitaji ya kocha wao.
“Nusu
ya wachezaji kiukweli mikataba yao inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu
huu, lakini uongozi umefanya mazungumzo ya awali na baadhi ya wachezaji wale
muhimu tunaowahitaji kwa ajili ya msimu ujao.
“Kikubwa tumepanga kukiimarisha kikosi chetu
kwa kuziboresha baadhi ya nafasi, tayari uongozi umefanya tathmini ya kila
mchezaji kwa kuangalia kiwango chake kabla ya kumsajili,” kilisema chanzo hicho.
0 COMMENTS:
Post a Comment