February 25, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm ambaye baadhi ya wachambuzi waliwahi kumponda na kudai hana lolote, eti ana umri mkubwa, sasa ameonyesha anaweza.


Licha ya kikosi chake kucheza vizuri, Mholanzi huyo ameacha rekodi ya pekee jijini Mbeya wakati alipokuwa akikiongoza kikosi chake katika mechi mbili za Ligi Kuu Bara dhidi ya Prisons na Mbeya City.

Katika mechi hizo, Yanga ilifanikiwa kuibuka na ushindi ambapo iliitandika Prisons mabao 3-0 na baadaye ikiinyuka Mbeya City mabao 3-1 na kufanikiwa kuondoka jijini humo.

Mechi hizo zimeifanya Yanga ikusanye pointi sita kwenye mechi mbili ugenini.

Rekodi ambayo Pluijm ameiacha jijini Mbeya ni ile ya kuiwezesha Yanga kuibuka na pointi sita jijini hapo kwa mara ya kwanza tangu mkoa huo uwe na timu mbili za ligi kuu.

Misimu mingine Yanga imekuwa ikiambulia pointi tatu au moja na kuna wakati mwingine ilikuwa ikiondoka patupu mkoani humo bila ya ushindi wa aina yoyote.

Hali hiyo ilimfanya Pluijm pamoja na baadhi ya viongozi wa benchi la ufundi la timu hiyo kushangilia kwa furaha ya ajabu baada ya kumalizika kwa mechi yao ya mwisho dhidi ya Mbeya City.

Mara ya mwisho Yanga ilishinda mkoani Mbeya zaidi ya miaka minne iliyopita.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic