February 12, 2015

KASEJA (KATIKATI) AKIWA MAHAKAMANI PAMOJA NA MWANASHERIA WAKE (KUSHOTO) NA MWANASHERIA WA YANGA, CHACHA.
 
Kesi inayomkabili aliyekuwa kipa wa Yanga, Juma Kaseja leo ilitakiwa kuanza kusikilizwa sasa imeahirishwa hadi Machi 10, mwaka huu.


Kesi hiyo ilipangwa kusikilizhwa katika Mahakama ya Kazi kitengo cha upatanishi lakini imeahirishwa na Hakimu Fimbo kufuatia ofisi ya Mawakili inayomuwakilisha Kaseja, Mbamba Advocates  kukumbwa na janga la kuungua moto na hivyo kupoteza nyaraka muhimu zikiwemo zilizokuwa zikihusu kesi hiyo.
Wakili aliyemuwakilisha Kaseja mahakamani hapo ni Nestor Mwenda kutoka Mbamba Advocate. Upande wa Yanga uliwakilishwa na Mkurugenzi wa Sheria wa timu hiyo, Frank Chacha.

Yanga inamdai Kaseja zaidi ya Sh milioni 200 kwa madai alikiuka mkataba.

Hata hivyo, Kaseja ndiye alikuwa wa kwanza kulalamika Yanga kuvunja mkataba kutokana na kushindwa kumlipa kwa wakati mwafaka.

Baadaye Yanga ilimlipa nay eye akaandika barua akitaka kurejea kazini lakini hakukuwa na majibu. Baada ya kuona ukimya huo, Kaseja aliamua kwenda katika mazoezi ya Yanga kuungana na wenzake, lakini akazuiwa na aliyekuwa Kocha wa Yanga, Marcio Maximo aliyesema lazima apate maelekezo kutoka kwa uongozi.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic