March 4, 2015


Uongozi wa Yanga umesema unatambua kwamba leoi Jumatano hakuna mechi yoyote ya Ligi Kuu Bara ambayo wanastahili kucheza.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha ambaye amesema kikosi chao kitaendelea na mazoezi kama kawaida mjini Bagamoyo.

Msemaji wa Yanga, Jerry Muro jana alisisitiza kwamba watapaleka timu Uwanja wa Taifa jijini Dar, leo kucheza dhidi ya JKT Ruvu.

“Tunajua hakuna mechi, nielewe hivyo na programu ya mazoezi inaendelea kama kawaida,” alisema Dk Tiboroha.
Alipoulizwa kuhusiana na kauli ya jana iliyotolewa na msemaji wa klabu yake, akasisitiza.

“Tunajua leo hakuna mechi, hadi Jumapili tutakapocheza dhidi ya Simba.”

Jana, Yanga walisisitiza wangepeleka timu uwanjani leo huku wakisisitiza kugomea mechi yao ya Machi 11 baada ya Bodi ya Ligi kuisogeza.

Yanga ilikuwa ikipinga kuahirishwa kwa mechi yao ya leo dhidi ya JKT na kusogezwa Machi 11, siku tatu kabla hawajashuka uwanja kuwavaa FC Platinum ya Zimbabwe katika Kombe la Shirikisho.



1 COMMENTS:

  1. Viongozi wa Siasa wawe wa siasa na wa soccer wawe wa soccer. Jerry amekuwa maarufu sana kupitia tasnia ya siasa. Mpira ubaki kuwa mpira asikurupuke na kuanza kuongea kama suala lenyewe hajalifanyia uchunguzi.
    Pia awe na mawasiliano ya karibu na katibu wake ili kuepuka kuwayumbisha watu.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic