Suala la mshambuliaji wa Yanga Amissi Tambwe kumshika
korodani beki wa Simba SC Murshid Juuko limepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu.
Uamuzi wa kulipeleka suala hilo kwenye
kamati ya nishamu umefikiwa baada ya Kikao cha Kamati ya Uendeshaji na
Usimamizi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania kilichoketi jumanne ya tarehe 24,
Machi 2015 jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho kimepitia taarifa mbalimbali
za michezo iliyochezwa na kutoa adhabu kwa wachezaji na vilabu vya Ligi Kuu ya
Bara.
Lakini suala hilo la Tambwe raia wa
Burundi kumshika beki huyo wa Simba kutoka Uganda, linakwenda kwenye kamati ya
nidhamu.
Tambwe alibambwa 'live' akifanya hivyo kupitia
picha iliyopigwa na gazeti namba moja la michezo nchini la Championi.
Picha ya Championi ilichapisha Tambwe
akiwa anamvuta korodani beki huyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment