April 25, 2015


Mambo magumu. Straika Said Bahanuzi wa Polisi Moro, amesema kuna kazi ngumu ya kuinusuru timu yake isishuke daraja msimu huu.

Polisi Moro inayomilikiwa na Polisi, inashika nafasi ya 12 katika msimamo wa timu 14 za Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 25 baada ya kucheza mechi 24 za ligi hiyo.

Bahanuzi anayecheza kwa mkopo katika timu hiyo akitokea Yanga, alisema: “Inaniuma kuona timu yangu ipo mkiani na kuna hali ya hatari ya kushuka daraja, tunahitaji kujituma ili kuibakiza timu katika ligi.”

“Kuna kazi kubwa ya kufanya kuhakikisha timu inabaki katika ligi, hasa kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu, vinginevyo aibu itatukuta.”


Hivi karibuni kocha Amri Said alijiondoa kuifundisha timu hiyo ambayo awali ilimtimua Adolf Rishard, hivyo sasa ipo chini ya John Tamba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic