April 16, 2015


Etoile du Sahel wametua nchini wakiwa tayari, usidhani hawajajiandaa kwa kuwa tayari wachezaji wawili raia wa Algeria wameandaliwa kuimaliza Yanga.

Washambuliaji hao wawili raia wa Algeria ambao  Baghdad Bounedjah na Kaddour Beldilali ndiyo wanaonekana kupewa jukumu la kubaki mbele kuimaliza Yanga.

Etoile kutoka Tunisia imepanga kujilinda sana katika mechi yake ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga jijini Dar es Salaam, kesho.

Pamoja na Waalgeria hao, wachezaji wengine wa kigeni ambao ni Franck Kom (Cameroon) na Alkhali Bangoura (Guinea).
Bangoura amekuwa akisifika kwa kupiga mashuti lakini Waalgeria hao wawili ndiyo mtambo wa mabao wa kikosi hicho cha Etoile.

Baghadad pia ana kasi, mjanja na mwepesi kupiga mashuti ya kushitukiza. Mabeki wa Yanga lazima wawe makini.

Ukiachana na wachezaji hao wanne, wachezaji wengine 14 waliobaki katika kikosi hicho ni raia wa Tunisia.
Yanga imeendelea kujifua vikali kujiandaa na mechi yake dhidi ya Etoile du Sahel ya Tunisia.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic