April 3, 2015


Hendrik Johannes Cruijff ‘Johan Cruyff’ ambaye ni kocha mkuu wa kikosi cha magwiji cha Barcelona anatarajiwa kutua leo saa moja asubuhi.


Magwiji hao wa Barcelona, watatua hapa nchini kwa ajili ya kuvaana na magwiji wa Tanzania katika mchezo utakaopigwa Aprili 11, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa waratibu wa ziara hiyo, Said Tully, amesema kocha huyo anatarajiwa kutua nchini tayari kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya magwiji wa soka waliowahi kuwika hapo zamani hapa nchini Tanzania.


Tully alisema wakati kocha huyo akitua, wachezaji wanaounda kikosi cha magwiji wa Barcelona, wanatarajiwa kutua Aprili 7, mwaka huu tayari kwa mechi hiyo.

Alikitaja kikosi cha magwiji wa Barcelona kinatarajiwa kuundwa na Patrick Kluivert, Deco, Luis Garcia, Gaizke Mendieta na Edgar Davids kabla ya siku ya pili yake kwenda Zanzibar baada ya kupata mwaliko wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Mohammed Shein.

Kwa upande wa kikosi cha magwiji wa Tanzania, kitaundwa na Mohammed Mwameja, John Mwansasu, Kali Ongala, Salvatory Edward, Yusuf Macho, Bita John, Victor Costa, Peter Manyika, Nassoro Bwanga na wengine wengi.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic