April 7, 2015

Uongozi wa kikosi cha Stand United umetamba kwamba ulijua kiungo Haruna Chanongo atakuwa msaada kwao kama ambavyo amekuwa akifanya.


Mkurugenzi wa Ufundi wa Stand United, Muhibu Kanu amesema waliamua kumuomba Chanongo ajiunge na kikosi chao akitokea Simba kwa kuwa waling’amua uwezo wake.

“Chanongo ni mchezaji mzuri, utaona sasa amekuwa msaada mkubwa kwetu kwa kushirikiana na wenzake.
“Sisi (Stand) tulijua atakuwa msaada mkubwa kwetu, mmeona namna anavyofanya kazi yake vizuri na kwa ufasaha,” alisema.

Simba ilimtoa Chanongo kwa mkopo baada ya kuonekana hana uelewano mzuri na uongozi.
Chanongo alikuwa kati ya wachezaji waliokuwa wakishutumiwa kuihujumu Simba na mwisho akapelekwa kwa mkopo.


Lakini sasa amekuwa msaada mkubwa kwa Stand United na jana aliibuka shujaa kwa kuifungia bao la ushindi dhidi ya Mtibwa Sugar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic