April 3, 2015

MASHABIKI WA MABINGWA TANZANIA BARA, AZAM FC AMBAO WANATETEA UBINGWA WAO HUKU WAKIPAMBANA NA VINARA WA LIGI HIYO, YANGA. SIMBA NDIYO WANAOSHIKA NAFASI YA TATU.
Bodi ya Ligi ambao ndiyo wasimamizi wa Ligi Kuu Bara, imeweka wazi kuwa kuanzia sasa, Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Tanzania (Takukuru) itazichunguza kwa kina timu tatu zinawania ubingwa wa ligi ambazo ni Simba, Yanga na Azam ili kukwepa upangaji wa matokeo.


Timu hizo ndizo zinazopigana kuwania ubingwa wa ligi kuu ambapo zinashika nafasi tatu za juu na ndiyo maana umuhimu mkubwa umeelekezwa kwao.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Ligi, Fatuma Abdallah alisema wamegundua kuwa ligi inapofikia mwishoni kumekuwa na matukio tata, hasa yanayoonekana kuhusishwa na upangaji wa matokeo.


Alisema kuwa tangu mwanzoni mwa msimu, Takukuru walikuwa wakiifanya kazi hiyo lakini katika kipindi hiki wameongeza nguvu kwa kuwa ndicho cha hatari zaidi kufanyika matukio hayo.


“Tumekuwa tukifanya kazi na Takukuru ya kuchunguza timu ambazo zinafanya hujuma katika ligi pamoja na kutoa rushwa kwa muda mrefu lakini sasa tumeongeza nguvu, hasa katika zile timu tatu za juu kwani hizo zinaweza kufanya vitendo vibaya ili waweze kutwaa ubingwa,” alisema Fatuma.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic