April 4, 2015

BASI WALILOKODI NA KULILINDA, HALAFU HAWAKULIPANDA....
 Na Theonas Mokiwa, Bulawayo
Yanga wameonyesha wamekomaa baada ya kung’amua mchezo mchafu waliokuwa wamefanyiwa na FC Platnum.


Dakika baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege Joshua Nkomo mjini Bulawayo, Zimbabwe, Yanga walikwenda kupanda basi la mashabiki.
Kilichowashangaza wahusika wa FC Platnum ni kuona wachezaji wa Yanga wakipanda basi lililotua mjini hapa likiwa na mashabiki kutoka jijini Dar es Salaam.

Tayari viongozi wa Yanga waliotangulia mjini hapa walikodi basi ambalo lilikuwa linalindwa muda wote.
BASI WALILOPANGIWA NA KULIKATAA....

Hata baada ya kutua kwa Yanga, hawakupanda basi hilo badala yake wakapanda lile la mashabiki aina ya Toyota Coasta ‘Mayai’.

Mashabiki nao wakapanda katika basi lililoletwa uwanjani na uongozi wa FC Platnum kwa ajili ya kuipokea Yanga.
Dereva wa basi lililoletwa na Platnum alikuwa akilalama kwamba alitumwa kubeba wachezaji na si mashabiki. Lakini haikusaidia.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic