May 13, 2015



Uongozi wa Free State Stars umekubali kumpa Mrisho Ngassa jezi namba 17 ambayo amekuwa akiitumia.
Hiyo inatokana na ombi la kiungo huyo wa zamani wa Yanga ambaye amejiunga na timu hiyo kwa ajili ya msimu ujao.


Akizungumza na SALEHJEMBE kutoka Afrika Kusini, 
Meneja wa Free State Stars, Motuba Mokoena amesema Ngassa ameomba kupewa jezi namba 17 ambayo amekuwa akiitumia kutokea Kagera Sugar, Yanga na Simba, pia kikosi cha Taifa Stars.

“Ngassa ameomba tumpe jezi na kumi na saba. Tumeona hilo linawezekana na tutalifanyia kazi.

“Naweza kusema ni uhakika tutampa jezi hiyo na kazi ya kuwakabidhi jezi mpya wachezaji wote itafanyika rasmi kesho (leo),” alisema.

Tayari Ngassa yuko Afrika Kusini ambako amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka minne.

Baada ya kukabidhiwa jezi, leo, Ngassa ataondoka kwenda kujiunga na kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kinachoshiriki michuano ya Cosafa inayofanyika nchini humo.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic