May 13, 2015


Baada ya kudaiwa kumwagiwa sumu katika vyumba vya kubadilishia nguo katika Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Ofisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amedai kuwa bado hali yake kiafya si nzuri licha ya kupata matibabu.


 Tukio hilo lilitokea wikiendi iliyopita wakati timu hiyo ilipokuwa ikivaana na Stand United uwanjani hapo na kudaiwa vyumba vya Ruvu vilipuliziwa vitu vinavyodaiwa kuwa na madhara na kumuathiri msemaji huyo na kocha wa timu hiyo, Mkenya, Tom Olaba.

“Naendelea vizuri kiasi lakini mwili wangu bado hauna nguvu na muda mwingine tumbo linavuruga, nimeshauriwa kunywa sana maji kuhakikisha nakuwa imara kabisa,” alisema Masau ambaye awali alipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Aghakhan ya Mwanza lakini kwa sasa yupo Dar akiendelea na matibabu.


Upande wa Olaba, kocha huyo alipozungumza na gazeti hili alisema: “Nina hasira sana, naomba nisiongelee masuala ya soka kwa sasa maana naweza kuongea kitu kibaya kikanisababishia makubwa, lakini naendelea na matibabu, nipo Morogoro, baada ya siku ile nililazimika kulazwa japokuwa kwa sasa naendelea vizuri.’

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic