May 2, 2015


Kila kukicha Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe anatamba kwamba atamsajili winga Simon Msuva wa Yanga, kumbe jeuri yake inatokana na wazazi wa mchezaji huyo.

Msuva aliliambia Championi Jumamosi kuwa, wazazi wake wote ni wapenzi wa Simba na kuna wakati akiwa Moro United kabla ya kutua Yanga baba yake Happygod Msuva alitaka kumpeleka Simba lakini ikashindikana.

“Baba alitaka kunipeleka Simba wakati ule, lakini kiongozi mmoja alikataa akiniambia nilikuwa mdogo ndipo nilipotua Yanga sasa bado mazungumzo yao na baba yanaendelea na wanajipa matumaini ya kunisajili kitu ambacho si sahihi,” alisema Msuva.

Mara kadhaa Hans Poppe amekaririwa na vyombo vya habari akisema lazima Msuva asajiliwe na Simba na kauli yake ameirudia hivi karibuni baada ya winga huyo kufikisha mabao 17 na kuongoza kwa ufungaji katika ligi kuu.

Kwa sasa Msuva yupo Tunisia na kikosi cha Yanga ambacho leo Jumamosi usiku kitacheza mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho na Etoile du Sahel jijini Sousse.
  


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic