May 20, 2015


Pamoja na kiungo wa Klabu ya Simba, Shabani Kisiga kuonyesha nia ya kurejea kundini kuitumikia klabu hiyo, uongozi wa timu hiyo umefungua kinywa na kudai kuwa hauwezi kumrudisha mchezaji huyo hata kwa dawa.


Uongozi huo umesema hayo baada ya kudai kuwa wamelisikia tamko la mchezaji huyo, lakini wao wanaona kama anawakejeli kwa sababu walimpa fursa mara mbili ya kujieleza na kushindwa kufika, kitendo kilichoashiria ni kama dharau.

Taarifa zinaeleza, Kisiga amekuwa akifanya juhudi za kuwashawishi viongozi ili arejee. Lakini amekataliwa katakata na sasa Simba inaangalia mipango ya kupata wachezaji watakaowaondoa walipo sasa.

"Lengo lilikuwa ni kutaka kutengeneza Simba iliyo imara, tuliamini Kisiga ni wachezaji wakongwe na watasaidia kuwaongoza vijana. Lakini haikuwa hivyo.

“Msimu ujao tunataka kuwa makini sana katika suala zima la usajili litakalozingatia zaidi nidhamu, kwani hata kama mchezaji ukiwa bora bila nidhamu ni sawa na bure,” kilieleza chanzo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic