May 20, 2015

MAKAPU (KUSHOTO) AKIPAMBANA NA AJIBU...
Huku kikosi cha Taifa Stars leo Jumatano kikitatarajiwa kushuka dimbani kumenyana na Madagascar katika mchezo wa pili wa michuano ya Cosafa inayofanyika nchini Afrika Kusini, timu hiyo inatarajia kukosa huduma ya kiungo mkabaji wa Yanga, Said Juma Makapu ambaye amerudishwa nchini kutokana na kuwa majeruhi.

Makapu, mashabiki mbalimbali wa soka hapa nchini wanamfananisha na kiungo wa timu ya Chelsea ya England, Nemanja Matic.

Akizungumzia juu ya jambo hilo, Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Selestine Mwesigwa, alisema mchezaji huyo amerudishwa nchini baada ya kuonekana ana majeraha yanayomsumbua na hayawezi kupona haraka na kupata fursa ya kuitumikia timu hiyo.

“Makapu anarudishwa Dar, ana majeraha ambayo aliyapata kwenye ligi na hivyo inaonekana hawezi kuitumikia timu hiyo huku Afrika Kusini,” alisema Mwesigwa.

Katika hatua nyingine, Mwesigwa alisema msimu ujao wa ligi kutakuwa na sheria pamoja na kanuni nyingi mpya baada ya kutoa fursa kwa timu zinazoshiriki kupendekeza maoni yao juu ya kipi kiongezwe na kipi kitolewe ili kunogesha ligi hiyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic