Baada ya kushindwa kuichezea CSKA Moscow
wakati alipofanya majaribio, taarifa zinaeleza huu ndiyo msimu wa mwisho kwa
mshambuliaji Mbwana Samatta katika kikosi cha TP Mazembe.
Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo amesisitiza
kwamba lazima mshambuliaji huyo Mtanzania ataondoka na kucheza Ulaya.
“Hata uongozi wa Mazembe nimeishazungumza
nao, lazima Mbwana ataondoka msimu huu. Atarudi tena CSKA kufanya mazoezi na
kuangalia nini kitafuatia.
“Unajua wakati ule alipata maumivu ya enka,
hakuweza kumalizia majaribio. Lakini kipande cha majaribio alichofanya,
kilikuwa na mafanikio makubwa.
“Hivyo TP Mazembe wameishakubali kwamba
watamuachia tena akafanye majaribio,” alisema Kisongo.
Samatta anatumikia mwaka wa mwisho wa
mkataba wake na Mazembe na ikishindwa kumuuza sasa, inaweza kumpoteza kama
ataondoka na yenyewe haitapata kitu.
Samatta amekuwa tegemeo la ushambuliaji
katika kikosi cha Mazembe hasa baada ya kuondoka kwa Tresor Mputu.
0 COMMENTS:
Post a Comment