May 13, 2015


Kocha wa zamani wa Simba, Mzambia, Patrick Phiri, ameweka wazi kuwa yupo tayari kuinoa Mwadui FC kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara endapo tu watakubaliana masuala ya mkataba.

Phiri ambaye aliipa Simba ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2009/10 bila kupoteza mchezo wowote, kwa sasa hana timu tangu atimuliwe na Simba mwishoni mwa mwaka jana na sasa yupo nchini kwao akijishughulisha na shughuli nyingine nje ya soka.

Phiri, amesema kuwa: “Kwa sasa sina timu, nipo ninaendelea na shughuli zangu binafsi, Mwadui sijaijua vizuri, ninaisikia juujuu tu, lakini mimi nipo tayari kufanya nao kazi endapo tutakubaliana masuala ya mkataba na maslahi kwani napenda kufanya kazi Tanzania.”

Mpaka sasa viongozi wa Mwadui FC wapo njia panda kama waendelee na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ ambaye alipata kazi kwa muda Coastal Union ya Tanga au waajiri kocha mwingine.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic