May 13, 2015


Wakati majaaliwa ya Kocha Goran Kopunovic raia wa Serbia yakiwa hayajulikani kuifundisha Simba, klabu hiyo imeweka wazi kuwa inatarajiwa kufanya usaili wa makocha wengine kutoka nchini Ufaransa, Bulgaria, Senegal na Serbia.


Simba imetoa tamko hilo kutokana na mkanganyiko wa masuala ya maslahi ya mkataba mpya kati ya Kopunovic na klabu hiyo ambapo imeelezwa kuwa Simba haipo tayari kuendelea kuwa naye ikiwa atashikilia msimamo wa kuhitaji maslahi wanayoona ni makubwa tofauti na bajeti yao.

Akizungumzia suala hilo Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba, Zacharia Hans Poppe, alisema mipango ya kuleta kocha mpya ipo ikiwa watashindwana rasmi na Mserbia huyo na kuzitaja nchi hizo kuwa ndiyo zinazoweza kutoa kocha wao.

“Ikiwa tutashindwana na Kopunovic, kuna makocha kutoka nchi nyingi tu, wapo kutoka Ufaransa, Senegal, Bulgaria na hata Serbia huko ambapo anatokea yeye,” alisema Hans Poppe.

Kuhusu usajili mpya ikiwa ni siku moja baada ya kutangaza wazi kutoendelea kuwa na beki Joseph Owino na Dan Sserunkuma kiongozi huyo alisema nako pia kuna wachezaji kutoka nchi kadhaa ambao wanajiandaa kuwaleta.

“Kuna wachezaji kutoka Ghana, Burundi, Kenya, Rwanda na Nigeria, kote huko tumeshapata maombi na mipango inafanyika kuja kufanya majaribio,” alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic