Kiungo wa Mbeya City, Peter Mwalyanzi amejiunga
na Simba ya Dar es Salaam.
Mwalyanzi amesaini mkataba wa miaka miwili
kuichezea Simba leo jijini Dar.
MWalyanzi amesaini mkataba huo mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, makamu wake Kassim Dewji na mjumbe Collins Frisch.
Simba imefanikiwa kumsainisha Mwalyanzi huku
Yanga ikiwa imemchukua kiungo mwingine wa Mbeya City, Deus Kaseke.
0 COMMENTS:
Post a Comment