May 12, 2015

 Kocha wa Bayern Munich, Pep Guardiola alionekana akizungumza mambo kadhaa na Lionel Messi wakati wa mapumziko.

Mechi kati ya Bayern Munich dhidi ya Barcelona ilikuwa mapumziko na wakati wanakwenda vyumbani wawili hao wakaanza kupiga stori.

Utafikiri Guardiola alikuwa akimuambia Messi: “Usiniue mwanangu.”
Maana Messi alifunga mabao mawili mjini Barcelona na kuisaidia timu yake kushinda kwa 3-0 ambazo zimesongesha mbele hadi kwenye fainali.

Kwani Bayern Munich imeshinda 3-2 lakini hazijaiwezesha kusonga mbele.
Kabla ya kutua Munich, Guardiola alikuwa Barcelona na mchezaji wake tegemeo alikuwa ni Messi.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic