Kiungo wa Simba, Jonas
Mkude ameanza majaribio katika klabu ya Bidvest ya Afrika Kusini lakini ana kazi
ya ziada kuonyesha kiwango cha juu zaidi kuliko Mrundi Papy Faty.
Faty ni Mrundi
anayecheza soka katika klabu hiyo ya Afrika Kusini na ndiye amekuwa tegemeo
katika uchezeshaji na ukabaji.
Hivyo lazima Mkude
apambane kuonyesha atakuwa na kiwango cha Faty au zaidi.
Faty alijiunga na timu hiyo mwaka 2012 akitokea APR ya Rwanda na amekuwa tegemeo katika kiungo cha timu hiyo.
Hivyo ni lazima kwa Mkude kuwashawishi Wasauz hao kwamba ana uwezo wa juu hata kama ni baadaye baada ya kutengenezwa, lakini waone kitu ndani yake.
Tayari ameanza mazoezi
kupambana kupata nafasi ya kuichezea klabu hiyo inayomilikiwa na Chuo Kikuu
kongwe cha Wits.








0 COMMENTS:
Post a Comment