Kocha
Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema ndiyo wanatengeneza kikosi na watu
wanapaswa kujenga subira.
Pluijm
amewatumia karibu wachezaji wake wageni wote kwa ajili ya kuwaangalia katika
mechi ya kirafiki dhidi ya SC Villa ya Uganda leo.
“Utaona
mechi imeisha kwa sare ya bila kufungana licha ya kwamba hakukuwa na mabao,
tumepata nafasi ya mkwaju wa penalty, lakini tumepoteza.
“Bado
tunatengeneza timu na unaona namna vijana walivyoonyesha mchezo mzuri.
“Bado
tuna mechi za kirafiki, muda wa mazoezi ambao pia utatupa nafasi ya kujua tuko
vipi.
“Sasa
ni mapema sana kujipima kwa kiasi cha kusema tuko vipi. Naweza kusema ulikuwa
mwanzo mzuri,” alisema Pluijm.
Licha
ya kujaza wachezaji wengi hasa mbele huku Deus Kaseke, Malimi Busungu na
Geofrey Mwashyuya bado waliweza kuonyesha kiwango kizuri.
0 COMMENTS:
Post a Comment